• Kuhusu Sisi
  • Tangaza
  • Mawasiliano
  • Privacy & Policy
Tanzania Monitor Swahili
Advertisement
  • Mwanzo
  • Uchumi
  • Biashara
  • Rasilimali
  • Utalii & Utamaduni
  • Siasa
  • Vifafanuzi
  • Multimedia
  • Michezo
  • English
No Result
View All Result
  • Mwanzo
  • Uchumi
  • Biashara
  • Rasilimali
  • Utalii & Utamaduni
  • Siasa
  • Vifafanuzi
  • Multimedia
  • Michezo
  • English
No Result
View All Result
Tanzania Monitor Swahili
No Result
View All Result
Home Habari Kuu

Wabunifu wa mitindo wapigwa msasa elimu ya fedha

Brighiter Masaki by Brighiter Masaki
January 30, 2026
in Habari Kuu
Reading Time: 2 mins read
0 0
0
Wabunifu wa mitindo wapigwa msasa elimu ya fedha
0
VIEWS
Share on FacebookShare on Twitter

DAR ES SALAAM: WABUNIFU wa mavazi, wanamitindo na washonaji nchini wamepewa mafunzo ya elimu ya fedha yenye lengo la kuinua biashara zao, kuongeza ajira kwa vijana na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Taifa.

Mafunzo hayo yalitolewa jana jijini Dar es Salaam katika Jukwaa la Mitindo Tanzania (Tanzania Fashion Forum), yaliyoandaliwa kwa ushirikiano wa taasisi za fedha na wadau wa tasnia ya ubunifu.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Jafari Hassanali, alisema tasnia ya mitindo inapaswa kubadilika kutoka kwenye kipaji na burudani na kuelekea kuwa biashara endelevu.

“Ubunifu tulionao lazima uendane na mifumo ya kibiashara ili kuushikilia na kuukuza uchumi wa Taifa. Tasnia ya mitindo ni sekta inayokua kwa kasi na ina uwezo mkubwa wa kutoa ajira, hasa kwa vijana,” amesema Hassanali.

Amewasisitiza wabunifu kutumia mikopo kwa uangalifu, akieleza kuwa mkopo ni nyenzo ya uwezeshaji na si mazoea.
“Unapokopa lazima ujue mkopo huo unaenda kufanya nini. Mkopo unapaswa kukamilisha oda au kuwekeza kwenye biashara, si kwa matumizi yasiyo na tija. Kukopa kwa ajili ya kula bata hakutakuza biashara,” amesisitiza.

Ameongeza kuwa kukopa fedha kwa ajili ya kulipa madeni mengine bila kuwekeza ni kuua biashara badala ya kuikuza.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Fashion Association Tanzania (FAT) na Muasisi wa Swahili Fashion Week, Mustapha Hassanali, alisema tasnia ya mitindo si suala la urembo pekee bali ni injini ya uchumi, ajira na utambulisho wa Taifa.

“Mitindo leo ni biashara, ni ajira, ni utambulisho wa Taifa na nafasi ya Tanzania katika dunia ya leo. Ubunifu bila mifumo, bila viwanda na bila miundombinu hauwezi kufika mbali,” amesema Mustapha.

Amesema kwa muda mrefu mitindo imeonekana kama maonesho pekee, badala ya sekta ya kiuchumi inayoweza kukuza biashara ndogo na za kati (SMEs), kuajiri vijana na kuongeza mapato ya Taifa.

“Dunia imetuonesha kuwa mitindo ya kimataifa ni sekta yenye thamani ya mabilioni ya dola. Nchi kama Italia, Uturuki na Morocco hazikufanikiwa kwa bahati mbaya, bali kwa kuitazama mitindo kama biashara na sekta ya viwanda,” ameeleza.

Mustapha amesema Tanzania ina vipaji vingi, lakini changamoto iliyopo ni kukosekana kwa mifumo madhubuti ya uzalishaji, masoko, mitaji na sera rafiki.

Ameongeza kuwa majadiliano hayo yanaendana na Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, inayolenga uchumi wa viwanda, ajira zenye tija kwa vijana na kunufaika na masoko ya kikanda na kimataifa kupitia AfCFTA na mpango wa Made in Tanzania.

“Mustakabali wa ubunifu wa Tanzania hautajengwe kwa kusubiri. Utajengwa kwa vitendo, kwa kuunganisha serikali, sekta binafsi, taasisi za fedha na elimu,” amesema.

Related Posts

Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa
Habari Kuu

Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

March 3, 2026
Serikali yatenga bilioni 29.5 kukabili ukame Longido
Habari Kuu

Serikali yatenga bilioni 29.5 kukabili ukame Longido

March 3, 2026
  • Trending
  • Comments
  • Latest

Hello world!

1

Shadow Tactics: Blades of the Shogun Review

0

macOS Sierra review: Mac users get a modest update this year

0

Hands on: Samsung Galaxy A5 2017 review

0
Samia aunga mkono uwekezaji wa sukari Tanzania

Samia aunga mkono uwekezaji wa sukari Tanzania

March 13, 2026
Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

March 3, 2026
Rwanda yashinikiza mfumo wa kikanda kudhibiti lugha za uchochezi

Rwanda yashinikiza mfumo wa kikanda kudhibiti lugha za uchochezi

March 3, 2026
Trump hotuba ya hali ya Taifa yakumbusha tukio la Pelosi

Trump hotuba ya hali ya Taifa yakumbusha tukio la Pelosi

March 3, 2026

Habari Mpya

Samia aunga mkono uwekezaji wa sukari Tanzania

Samia aunga mkono uwekezaji wa sukari Tanzania

March 13, 2026
Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

March 3, 2026
Rwanda yashinikiza mfumo wa kikanda kudhibiti lugha za uchochezi

Rwanda yashinikiza mfumo wa kikanda kudhibiti lugha za uchochezi

March 3, 2026
Trump hotuba ya hali ya Taifa yakumbusha tukio la Pelosi

Trump hotuba ya hali ya Taifa yakumbusha tukio la Pelosi

March 3, 2026
Safari za ndege wanaohama zatoa funzo kwa dunia isiyo na mipaka

Safari za ndege wanaohama zatoa funzo kwa dunia isiyo na mipaka

March 3, 2026
Vifo vya wanajeshi vyasababisha Chad kufunga mpaka

Vifo vya wanajeshi vyasababisha Chad kufunga mpaka

March 3, 2026
Tanzania Monitor Swahili

Jukwaa la kimataifa la lugha nyingi linaloelezea uchumi wa Tanzania, uwekezaji, utamaduni, utalii na michezo kupitia taarifa za kuaminika zinazotokana na takwimu.

Tufuatilie

Vinjari kwa mgawanyo

  • Biashara
  • Habari Kuu
  • Michezo
  • Rasilimali
  • Siasa
  • Uchumi
  • Uncategorized
  • Utalii & Utamaduni
  • Vifafanuzi

Habari Mpya

Samia aunga mkono uwekezaji wa sukari Tanzania

Samia aunga mkono uwekezaji wa sukari Tanzania

March 13, 2026
Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

Madai kupiga risasi Oktoba 2025 kuchunguzwa

March 3, 2026
  • Kuhusu Sisi
  • Tangaza
  • Mawasiliano
  • Privacy & Policy

© 2026 Tanzania Monitor.

Welcome Back!

Login to your account below

Forgotten Password?

Retrieve your password

Please enter your username or email address to reset your password.

Log In

Add New Playlist

No Result
View All Result
  • Mwanzo
  • Uchumi
  • Biashara
  • Rasilimali
  • Utalii & Utamaduni
  • Siasa
  • Vifafanuzi
  • Multimedia
  • Michezo
  • English

© 2026 Tanzania Monitor.

Are you sure want to unlock this post?
Unlock left : 0
Are you sure want to cancel subscription?
Go to mobile version