DODOMA, Tanzania: Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Februari 5, 2026, imefanya kikao na Makamu wa Rais mstaafu, Dkt. Philip Mpango, mjini Dodoma.
Katika kikao hicho, Tume na Dk. Mpango wamejadili chanzo cha matukio ya uvunjifu wa amani, athari zake kwa watu, mali na miundombinu, pamoja na kutoa ushauri wa namna ya kuzuia na kushughulikia matukio kama haya katika siku zijazo.
Tume hiyo, inayosimamiwa na Jaji mstaafu, bado inaendelea kukutana na makundi mbalimbali, yakiwemo waathirika wa matukio hayo, ili kukusanya taarifa kamili za tukio la uvunjifu wa amani lililotokea Oktoba 29, 2025.
Lengo la kikao hiki ni kuhakikisha uchunguzi unafanikwa kikamilifu, huku jamii ikipewa nafasi ya kutoa maoni na uzoefu wao, ili matukio kama haya yasitoke tena nchini.








